Idara ya Afya inazidi kumshukuru Mungu kwa kuwezesha vitengo vyake mbali mbali kutekeleza vyema shughuli zake kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi 2018.
Mpaka kufikia tarehe ya taarifa hii…
- Idara ya Afya ina Zahanati 7 zinazofanya kazi.
- Kituo cha Afya 1.
- Hospitali 3.
- Taasisi 2 za kutolea mafunzo (Training Institutions ) ambazo ni ALMC Surgery Residency programme na ALMC Nursing school.
Sambamba na vituo tajwa hapo juu, Idara inayo Miradi mbali mbali kama vile Mradi wa kuzuia na kupambana na Ukimwi (USAID Boresha Afya), Huduma ya Faraja na Tiba Shufaa (Hospice & Palliative Care service), Mradi wa Fistula, mradi wa kutunzia wagonjwa waliorekebishwa mifupa kwa njia ya upasuaji (Plastic surgery) na Mradi wa kuzuia na kudhibiti magonjwa ya macho (Eye Mobile Clinic).
Idadi ya watumishi katika vituo vyetu ni 732. Mchanganuo wa watumishi hao kutokana na kada zao ni kama ifuatavyo:-
- Madaktari 71.
- Wauguzi 208.
- Wengineo 453.