Neno La Utangulizi Kutoka Kwa Askofu

KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Kati, inamshukuru Mungu kwamba katika hekima yake isiyopimika, na kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo, ametuunganisha waumini wake wote ulimwenguni kuwa wamoja.

Kwa njia hiyo, tunaweza kushirikiana pamoja na kufanikishwa katika mambo mengi. Dayosisi yetu inajihusisha na huduma mbalimbali za kijamii, kiroho, kiuchumi na kiakili kupitia idara za Misioni na Uinjilisti, Jinsia, Diakonia, Ibada na Muziki, Afya, Elimu, Mipango, Fedha na Utawala. Dayosisi ina Majimbo Saba Kanisa Kuu na Sharika 137.

Tovuti hii kwa namna iliyo bora, inaeleza mambo yote yanayofanywa na Dayosisi hii pamoja na Uongozi wake. Tunakukaribisha kutembelea Tovuti yetu.

“Tazama jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja”. Zab 133:1.

Wenu,

Askofu Dkt. Godson Abel Mollel

Mkuu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Kati.

KUHUSU SISI

Dayosisiya Kaskazini kati ya KKKT ilianza mwaka 1973, wakati huo ikijulikana kwa jina la  Sinodi Mkoani Arusha, iliyoongozwa na Mchungaji Mesiaki Kilevo; akiwa kiongozi wa kwanza wa Sinodi ikiwa na Washarika 30,000, Sharika 20 na Mitaa 110. 

Kiongozi wa Pili wa Sinodi alikuwa hayati Askofu Dkt Thomas Olmorijoi Laiser kuanzia mwaka 1980 hadi mwaka 1986.

Mwaka huo wa 1986 Sinodi ilibadilika kuwa Dayosisi Mkoani Arusha na Askofu wa kwanza akawa hayati Askofu Dkt Thomas Olmorijoi Laiser.  

Mwaka 2010 Dayosisi Mkoani Arusha ilibadili jina na kuwa Dayosisi ya Kaskazini Kati, baada ya Serikali ya awamu ya tatu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kuamua kuugawa Mkoa wa Arusha na kutokeza mikoa ya Arusha na Manyara.

idara

IDARA MBALIMBALI

IDARA YA ELIMU

IDARA YA AFYA

IDARA YA RASLIMALI WATU

IDARA YA HAZINA

Idara ya Miradi na Mali

ARUSHA CORRIDOR SPRINGS HOTEL

ARUSHA LUTHERAN MEDICAL CENTRE

Utangulizi

Idara ya Miradi   na  mali  inahusika na usimamizi wa Miradi ya huduma kwa jamii na   ya uchumi.Miradi ya jamii ni ile miradi inayohusika katika kuboresha hali ya maisha ya jamii.

Miradi ya uchumi

Kwa wakati huu Dayosisi ina Hotel ya Arusha Corridor Springs kama mradi wa kiuchumi pamoja na Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre.

MIRADI YA JAMII

Dayosisi imewajengea wamama walezi pekee/wajane nyumba zaidi ya 145 kwa mkopo wa bei nafuu na bado inaendelea kujenga...

Idara ya Elimu

Utangulizi

Dayosisi ya Kaskazini Kati ina taasisi za elimu ambazo zimegawanyika katika mkundi makuu matatu.

Shule za msingi

Shule za msingi 3 zinazoanza na madarasa ya awali ambazo ni Kimandolu, Ilboru na Tetra (Enkarenarok)

Shule za sekondari

Shule za sekondari 8 ambazo ni Kimandolu,Tetra, Ngateu, Ekenywa, Enaboishu, Peace House sekondari, Moringe na Sekondari ya wasichana wa Maasae.

Vyuo vya Ufundi

Vyuo vya Ufundi 2 ambazo ni Chuo cha Kilimo, mifugo na Ufundi-BACHO na Chuo cha ufundi kilichoko Olokii.

PEACE HOUSE SECONDARY SCHOOL

ENABOISHU SECONDARY SCHOOL

Ijue Idara Ya Jinsia Katika Dayosisi ya kaskazini Kati

Idara hii inashughulikia maendeleo na mambo yote yanayohusu Wanawake,Wanaume,Vijana na Watoto.

Menejimenti ya Dayosisi

Wasiliana Nasi